Mon, 12 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kikosi cha Simba SC kimefanya mazoezi ya mwisho katika Uwanja wa CCM Kirumba kujiandaa na mchezo wa kesho wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Geita Gold.
Wachezaji wote wameshiriki mazoezi hayo na wapo kwenye hali nzuri tayari kwa mchezo wa leo.
Simba inategemea kupata upinzani mkubwa kutoka kwa Geita lakini hata hivyo wamejipanga kuhakikisha wanaondoka na alama zote tatu.
Hakuna mchezaji yoyote ambaye watamkosa katika mchezo wa kesho kutokana nakuwa majeruhi au kutumikia adhabu ya kadi hivyo wapo kamili kuivaa Geita leo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live