Baada ya mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia kati ya Tanzania dhidi ya Morocco jana, mashabiki wengi walikuwa wanatamani kupata picha na baadhi ya mastaa wa timu ya taifa ya Morocco wanaocheza klabu kubwa Ulaya.
Miongoni mwa wachezaji waliokuwa wakisubiriwa na mashabiki wengi ni Sofyan Amrabat wa Manchester United na Achraf Hakimi wa PSG ili kupata fursa ya kupiganao picha kwa ajili ya kumbukumbu.
Walinzi wa Kampuni ya ulinzi ya K4S Security walifanya kazi ya ziada kuhakikisha wachezaji hao hawapati usumbufu ambao ungesababishwa na msongamano wa mashabiki waliokuwa wakitamani kupiga nao picha.
Morocco iliondoka na alama zote tatu (3) kwenye Uwanja wa Mkapa baada ya kushinda kwa magoli 2-0 ikiwa ni mchezo wao wa kwanza wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2026.