Baada ya kukamilisha na kutangaza usajili wa kiungo mpya, Fabrice Ngoma, tayari kikosi cha Simba kimeenea kwa idadi ya wachezaji wa kigeni kuelekea msimu ujao 2023/24.
Kwa mujibu wa kanuni za Shirikisho la Soka Tanzania, Klabu inatakiwa kusajili wachezaji wa kigeni wasiozidi 12 kwa msimu husika wa mashindano, ambapo mapaka sasa idadi hiyo kwa Simba imetimia.
Endapo Simba watahitaji kusajili kipa wa kigeni kama tetesi zinavyodai kuchukua nafasi ya Aishi Manula ambaye ni mgonjwa, ama mchezaji yoyote anayecheza nafasi za ndani ya uwanja, wanahitaji kumwondoa mchezaji mmoja wa kigeni ili kuruhusu usajili huo ukamilike.
Wachezaji 12 wa kigeni wa Simba msimu ujao mpaka sasa ni hawa;
Clatouas Chota Chama - Zambia
Moses Phiri - Zambia
Peter Banda - Malawi
Pape Ousmane Sakho - Senegal
Sadio Kanoute - Mali
Aubin Kramo Kouamé - Cote d'Ivoire
Jean Toria Baleke Othos - Congo DR
Henock Inonga Baka - Congo DR
Fabrice Luamba Ngoma - Congo DR
Willy Essomba Onana - Cameroon
Saidi Ntibazonkiza - Burundi
Che Fondoh Malone Jr. - Cameroon.
Nani atoke ili aingine kipa?