Kiungo wa Manchester United, Mason Mount atakuwa nje ya uwanja kwa wiki kadhaa baada ya kupata jeraha la msuli kwenye mchezo uliopita dhidi ya Brighton ambapo Mashetani hao Wekundu walipoteza 2-1.
Akithibitisha hilo Mount ameoneshwa kukerwa na hali hiyo ya kuwa nje kwa majeraha huku akiwatoa wasiwasi mashabiki wake kuwa atafanya kila liwezekanalo kurejea katika hali bora na kuisaidia timu.
“Wakati wa mchezo uliopita nilipata tatizo dogo la misuli. Nitakuwa nje kwa michezo michache. Nilifanya kazi kwa bidii ili kurudisha utimamu wangu mahali panapohitajika, nilijihisi imara na tayari” — Amesema Mount.