Moja ya taarifa kubwa ambayo Mashabiki wa Yanga huenda wanaisubiri kwa hamu katika dirisha hili kubwa la usajili ni kujua hatima ya Mshambuliaji wa klabu yao Fiston Mayele.
Mayele yupo Tanzania lakini bado hakuna taarifa za uhakika kama ataendelea kusalia katika kikosi cha wananchi katika msimu ujao.
Kila siku kumekuwa na tetesi zinazozuka juu ya uelekeo wa Mfungaji huyo bora wa Ligi Kuu Bara 2022/23 na Kombe la Shirikisho Afrika.
Kwa Mashabiki wa Yanga kwa sasa taarifa za Mayele kusalia katika kikosi cha Yanga na kusaini mkataba mpya ni habari kubwa zaidi ya kutambulishwa kwa mchezaji mpya anesubiriwa atakaevaa jezi namba 6
Wananchi hebu toeni maoni yenu mnasubiri habari gani kwa hamu kwa sasa?