Wed, 6 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wenyeji, Mashujaa FC wamelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na jirani zao, Tabora United katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Jana Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.
Mashujaa FC walianza kupata bao kupitia kwa Jeremanus Josephat dakika ya 11, kabla ya Eric Okutu kuisawazishia Tabora United dakika ya 47.
Kwa matokeo hayo, Mashujaa wanafikisha pointi tisa katika mchezo wa 10, ingawa wanabaki nafasi ya 15, wakati Tabora United inafikisha pointi 15 na kusogea nafasi ya saba baada ya kucheza mechi 11.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: