Wed, 1 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Azam FC itakuwa na kibarua kigumu wakati itakapokuwa inacheza na Mashujaa saa 10:00 jioni kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma huku timu zote zikiwa na kumbukumbu ya kupoteza michezo yao miwili mfululizo.
Mechi ya mapema saa 8:00 itazikutanisha Singida Big Stars itayokuwa nyumbani kucheza dhidi ya Ihefu kwenye Uwanja wa Liti, mjini Singida.
Timu zote zinakutana zikitoka kupoteza michezo yao ya mwisho na Singida ilichapwa mabao 2-0 na mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara Yanga kwenye Uwanja wa Benja-min Mkapa, jijini Dar es Salaam sawa na Ihefu pia iliyochapwa na Simba 2-1.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live