Tue, 5 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kama watazichanga karata zao vizuri basi Mashujaa FC leo wataibukia kwa Tabora United kwani watakuwa kwenye dimba lao la nyumbani.
Mashujaa ambao kwa sasa wapo nafasi ya 15 kwenye msimamo na alama zao 8, wamekuwa na matokeo mabaya mfululizo licha ya kuanza ligi vizuri na watamkabili Tabora ambaye yupo nafasi ya 9 kwenye msimamo na alama zao 14.
Mashujaa wana takriban mechi tano mfululizo wametoka kupokea kipigo pasi na kupata ushindi. Kazi wanayo leo majira ya saa 10: 00 jioni katika uwanja wao wa nyumbani Lake Tanganyika.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live