Wed, 26 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Mashujaa FC iliyopanda Ligi Kuu ya NBC, inaendelea kufanya sajili kila eneo kwa lengo la kuhakikisha wanafanya vyema msimu 2023/24.
Mpaka sasa Klabu ya Mashujaa imefanya sajili kadhaa lakini imeshanyakua wachezaji watano kutoka katika Timu ya Ruvu Shooting iliyoshuka daraja msimu uliopita na kuzidi kuidhoofisha Timu hiyo.
Wachezaji watano waliosajiliwa na Mashujaa kutoka Ruvu ni pamoja na Abdallah Rashid, Frank Nchimbi, Zuber Dabi, Kindamba na Mgandila Shaban.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live