Thu, 9 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchambuzi wa soka Bongo, Shafii Dauda amewataka mashabiki wa Simba kuacha kuandamana kwani kama kuandamana wangeandamana Manchester United kwani wao wanapitia nyakati ngumu.
Shafii amewataka mashabiki wa Simba wawe kitu kimoja wakaisapoti timu yao.
“Mambo ya kuandamana hayana mpango wowote, kama kuandamana wangeandamana Manchester United huko kwa hiki wanachopitia, kazi ya shabiki ni kuisapoti timu yake, Manchester United wanafungwa na mechi ijayo wanaenda uwanjani kwa wingi ule ule," alisema Shifii.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live