Mwanasoka wa Zambia Lameck Banda na mchezaji mwenzake wa Lecce Samuel Umtiti walinyanyaswa kwa ubaguzi wa rangi walipowatembelea mashabiki wa Lazio katika mchezo wa Serie A ya Italia Jumatano.
Mwamuzi alisimamisha mchezo katika kipindi cha pili kwa sababu ya dhihaka za kibaguzi, shirika la habari la AFP linaripoti.
Umtiti mchezazaji wa kimataifa wa Ufaransa ndiye alikuwa mlengwa mkuu wa unyanyasaji huo. Lecce, ambaye ilishinda 2-1, baadaye iliwasifu mashabiki wao kwa kujibu unyanyasaji huo kwa kuimba jina la Umtiti. "Nyimbo za kibaguzi zilizamishwa na zile za kutia moyo," kilabu kilisema kwenye ukurasa wao wa twitter.