Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mashabiki Simba wamvaa Robertinho

Bocco Robertinhooo Mashabiki Simba wamvaa Robertinho

Sat, 28 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Katika toleo la juzi Alhamisi, mchambuzi wetu Oscar Oscar aliandika uchambuzi uliokuwa na kichwa cha habari “Kwa Bocco... Robertinho aache kutudanganya”. Mashabiki kupitia namba yetu ya simu walituma maoni kwa mamia wakionyesha hisia tofauti lakini wengi wakitoa ya moyoni kwamba wanataka kuona mabadiliko kikosini. Kutokana na muitikio kuwa mkubwa tumechapisha baadhi ya meseji hizo;

Bocco awekwe benchi

KWA usajili wa Simba hii ya msimu huu hata timu akipewa Juma Mgunda na Seleman Matola tunachukua ubingwa wa Ligi Kuu Bara, aache kumtumia John Bocco awatumie Moses Phiri na Jean Baleke, Simba inaweza kufunga mabao zaidi ya matano katika mechi moja.

Ajaba Ndogoro

Umri umemtupa

Umri wa Bocco ni kweli umepita na Phiri anabaniwa sana.

Fredy wa Arusha

Uwezo umepungua

Uko sahihi uwezo wa Bocco umepungua.

Modestus, Kigamboni

Kocha aachane na Bocco

Kocha anatuongopea na kuiabisha Simba wakati kuna wachezaji wengi kama Shabani Chilunda na Bocco na wengine ambao hawapi nafasi na wangeweza kuisaidia timu.

Mohamed, Morogoro

Umelenga, Bocco sio

Mwanangu umelenga penyewe Simba imekosa kusonga mbele kwa tatizo moja tu na la kocha kutowaanzisha wachezaji muhimu kwani mbele anatakiwa awe Clatous Chama, Phiri, Baleke, Saido Ntibanzonkiza, Kibu adui hawezi kuchomoka.

Kasongwa, Kyela Mbeya

Awe Baleke, Phiri

Kwa nini mechi kubwa za kimataifa kocha anamwanzisha Bocco badala ya wachezaji wenye uwezo na ni vijana kama Baleke na Phiri na wanaweza kuleta matokeo ya haraka ila wanakuwa benchi.

Masanja, Simiyu

Bocco asubiri matokeo

Ombi langu kwa benchi la ufundi ni waanze sasa kuwatumia wakina Phiri na Baleke, Bocco wampumzishe apewe nafasi timu ikiwa na matokeo. Kila la Kheri kwenye mechi ya Ihefu.

Msamara, Ubungo

Simba tunawaheshimu

Nawapongeza wachezaji wa Simba kwa kuheshimiana na kulinda walichopata.

Paul Tobiko, Kiteto

Huyu sio Bocco yule

Ndugu yangu pole na kazi ni kweli ndugu yetu kipenzi cha mashabiki Bocco sio yule wa Azam ila naomba aheshimiwe na kupewa maua yake na apewe hata timu ya watoto awakuze.

Andrew Mwangosi, Mbeya

Kocha awe makini

Ushauri kwa kocha wa Simba aangalie kwa upya maamuzi yake ya kumuanzisha Bocco kipindi cha kwanza. Jackson Elia, Arusha

Viongozi wanampanga Bocco

Bocco kuwa nje inawezekana kuwa ni maamuzi ya viongozi kumtaka acheze maana kwa akili ya kawaida huwezi kumuacha Phiri nje na kumchezesha yeye.

Muhsin Mkami, Ilala

Inauma sana

Roho inaniuma Phiri anawekwa benchi kocha atamfanya apoteze ubora wake wa kufunga.

Jamal Kihiyo

Msipoe-lewa tutaa-ndamana

Kama kocha hataacha kum-chezesha Bocco sisi kama mashabiki tutaanda-mana mbona wapo wakina Chilunda na Phiri.

Abedy Gidion, Mwanza

Bocco abaki kwenye historia

Kocha asiangalie historia ya nyuma ya Bocco kweli tunamheshimu lakini kwa sasa wamuache tunaumia kwa sababu uwezekano wa kumtoa Al Ahly tulikuwa nao kabisa.

Ruhondo

Phiri apewe nafasi

Kweli Bocco kachoka wapewe nafasi Baleke na Phiri.

Babu Mbishi, Ilala

Kocha anammaliza Phiri

Naumia sana kuona kocha anaua uwezo wa Phiri.

Miriam Karia

Robertinho ana shida

Simba kocha anashida maana anawanyima wengine nafasi na kuwapa wazee.

Said, Dar

Kocha anawaridhisha mabosi

Kocha aache kusikiliza viongozi maana anacheza na akili zao ili kuwaridhisha ila kuna wachezaji wazuri zaidi ya Bocco.

Peter Kibula, Kimara

Akae benchi tu

Bocco aanze benchi na Phiri aanze kocha akifanya hivyo tunatoboa.

Yusuf, Morogoro

Kocha asipobadilika, tutambadilisha

Timu ikianza kupoteza kwaajili ya maamuzi yake mabaya basi ajue mashabiki watamzomea na kutomtaka tena hivyo asipobadilika watu watambadilikia.

Raymond Mwasemeleke, Tandika

Kocha anatudanganya

Naungana na nawe ulichapisha mawazo yako yakibebwa na kichwa cha Bocco, kocha aache kutudanganya na acheze wachezaji wengine.

Maswale, Msamvu Morogoro

Bocco ana kitu

Kwenye maoni kuhusu Bocco, sio kwamba asipangwe kucheza kabisa na haiwezekani akawa hana hata vichache vya manufaa wakati aliisaidia timu Algeria kuliko hata Shomari Kapombe na Mohamed Hussein ‘Tshabalala’.

Msomaji wetu

Bocco hayuko fiti

Naungana na wewe kwa asilimia 100 kocha anatudanganya anawaweka nje washambuliaji wa maana anamuweka Bocco ambae hayuko fiti.

Msomaji wetu

Shida ni Robertinho

Usiwe mnazi, achambuliwe kwanza Kocha ndio mbovu kuliko huyo Bocco.

Msomaji wetu

Ribertinho awe mkweli

Nakuunga mkono kuhusu Bocco, kocha asitudanganye.

Msomaji wetu

Bocco anatupa presha

Naunga mkono juu ya Bocco kwani umri wake umeenda sasa na mashabiki tukiona amepangwa matumbo yanapata moto fuatilia hata vibandani au uwanjani utagundua hilo.

Msomaji wetu

Bocco apewe nyepesi

Nimekupenda Oscar kwa uchambuzi wako, ila ningetamani kuona Bocco anapewa mechi nyepesi ili amalize safari ya soka kwa heshima maana kuna mashabiki wengine watasahau aliyoyafanya na kuanza kumzomea hali itakayoshusha thamani yake. Msomaji wetu

Asingemwanzisha Bocco

Kocha alikosea kumuanzisha Bocco na Ahly kwani hesabu zake za kipindi cha kwanza ndicho kilichoifelisha Simba kukosa matokeo wala sio sababu ya ukubwa wa wapinzani waliokutana nao.

Msomaji wetu

Mashabiki tuna shida

Mashabiki tuna matatizo tulimsakama Kibu Denis hadi akashuka uwezo hivyo hata Bocco tumuache ijapokuwa ni kweli kuwa kuna vitu vimepungua kwake.

Msomaji wetu

Onana, Bocco shida

Kweli Onana hana umakini bado na Bocco hamna kitu.

Msomaji wetu

Bocco waachie Phiri, Baleke

Una mawazo mazuri ya kujenga Simba yetu amwachie Baleke na Phiri pia awaachie Onana na Saido pia umri umeenda aingizwe dakika 70.

Msomaji wetu

Viongozi Simba ndo shida, dirisha dogo Simba wamuache Bocco akafundishe vijana na viongozi wa Simba pia ni matatizo kwani inaonekana wana vipaumbele vyao. Msomaji wetu

Ni kweli eti, mimi ni shabiki tangu 1970 na ulichosema kuhusu Bocco ni cha kweli. Msomaji wetu

Bocco awaachie wengine

Bocco anawabania wengine nafasi kwani ameshapitwa na wakati. Msomaji wetu

Viongozi Simba wanazingua

Ni swala la Viongozi kwani wanampangia kocha wachezaji wa kucheza maana kwa uzoefu tu wa kawaida huwezi kumchezesha Bocco kipindi cha kwanza.

Msomaji wetu

Kocha unazingua, kocha anatukera sana mashabiki kwani hawa wengine wanashida gani?

Msomaji wetu

Kocha anatudanganya, sio Bocco tu hata Onana huwezi kuwaingiza hao na kumuacha Phiri benchi huo ni uharibifu wa timu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live