Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mashabiki Chelsea watakiwa kumpa muda Nicolas Jackson

Nicolas Jackson During A Chelsea Match Mashabiki Chelsea watakiwa kumpa muda Nicolas Jackson

Tue, 26 Sep 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mashabiki wa Chelsea wametakiwa kumpa muda Nicolas Jackson, na mwanzo wake wa maisha katika klabu hiyo ikilinganishwa na Didier Drogba.

Nicolas Jackson mwenye umri wa miaka 22 alijiunga na Chelsea kwa uhamisho wa pauni milioni 32 kutoka Villarreal msimu wa joto.

Jackson alivutia sana kwa kufumania nyavu mara mbili kabla ya msimu mpya kuanza, lakini amefunga mara moja tu katika mechi sita za Ligi Kuu ya Uingereza.

Aling’ara katika mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu ya Uingereza katika sare ya 1-1 dhidi ya Liverpool mwezi Agosti, na anaendelea kuonyesha mwanga wa uwezo wake wa kweli.

Fowadi huyo alishindwa kufunga bao katika kipigo cha 1-0 dhidi ya Aston Villa mwishoni mwa wiki, lakini beki wa zamani wa Chelsea Scott Minto anaamini anaweza kuwa mmoja wa wachezaji bora kama Drogba.

Tembelea duka la ubashiri-Meridianbet kutandika jamvi lako kwa odds kubwa.

Beki huyo wa zamani wa Chelsea alisema: “Nampenda sana Nicolas Jackson, na nadhani ukimpa muda, atakuwa mshambuliaji bora wa Premier League.

“Ninamtazama na nguvu zake, ana kasi, ana uwezo wa kuwapita mabeki, ni mkali na anataka kufanyia kazi timu.

“Kitu pekee anachopungukiwa kwa sasa ni kupachika mpira wavuni.

“Didier Drogba, alipokuja Chelsea kwa mara ya kwanza, baadhi ya mashabiki hawakuwa naye mara moja. Alichukua muda kuonesha.

“Ninampenda sana [Jackson], na ninakuambia ni mchezaji mzuri sana.”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live