Tue, 11 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Staa wa zamani wa Arsenal, Emmanuel Petit amesema mashabiki wa miamba hiyo ya Emirates watafurahia usajili wa Declan Rice na wala hawatajali bei ya kiungo huyo.
Kinachoelezwa ni Arsenal imefikia makubaliano na West Ham United kulipa Pauni 105 kwa ajili ya kunasa saini ya kiungo huyo mkabaji, Rice.
Ada hiyo ya uhamisho itaweka rekodi kwa England, ikiwa ni kubwa kwa usajili wa ndani kwenye Ligi Kuu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live