Thu, 7 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mashabiki wa klabu ya Arsenal nchini England wameomba kupitisha bakuli ili wapate pesa za kuwaongeza Westham United kwenye mauzo ya Declan Rice.
Hayo yanakuja baada ya mashabiki hao kukoshwa na uwezo wa nyota huyo tangu ajiunge na kikosi hicho na kuhisi mkurugenzi wa michezo wa klabu hiyo Edu na wenzake waliionea Westham katika dili hilo.
Mashabiki wanadai kuwa kwa uwezo alionao Rice hawakupaswa kumnunua kwa £ 105 Million.
Tayari Arsenal wameshaanza mbwembwe je wataubeba Ubingwa? Tupe maoni yako
Chanzo: www.tanzaniaweb.live