Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Masau Bwire atangaza hali ya hatari Ligi Kuu, atambulisha 'Double K'

Masau JKT TZ Masau Bwire

Tue, 1 Aug 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ofisa Habari wa Klabu ya JKT Tanzania Masau Bwire amevipa Vilabu tahadhari kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu 2023/24.

Masau ambae alikuwa na Klabu ya Ruvu Shooting kwa miaka mingi kabla ya msimu uliopita Ruvu kushuka daraja.

Masau amesema wamekuja na mtindo mpya wa kutoa vipigo kwa wapinzani wao msimu ujao.

“Msimu ujao JKT Tanzania tunakuja na Double K, ‘Kichapo Cha Kizalendo’, yaani tunakupiga husikii maumivu lakini ndo unapigwa hivyo”

Klabu ya JKT Tanzania makao makuu ya klabu hiyo yatakuwa Dar es Salaam na siyo Dodoma kama ilivyozungumzwa awali.

JKT Tanzania imepanda daraja kucheza Ligi Kuu msimu ujao.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live