Afisa Habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwire, amesema wanaziangalia mechi zao nne zilizosalia kwenye Ligi Kuu ya NBC kwa jicho la tofauti ili waweze kujinasua nafasi ya pili kutoka mkiani kwenye msimamo.
Masau ameyazungumza hayo wakiwa kwenye maandalizi wa mchezo wao wa kwanza kati minne iliyobaki dhidi ya Azam FC mchezo utakaochezwa kesho Aprili 22, 2023.
"Tunaingalia hii michezo yetu kwa namna tofauti sana kuliko watu wanavyofikiri kwamba tunashuka daraja, sisi tutacheza vizuri ili kujitoa huku kwenye nafasi ya hatari tulipo," alisema Masau.
Michezo iliyosalia kwa Ruvu mbali na Azam, watakipiga na Simba SC, Dodoma Jiji na Singida Big Stars.