Klabu ya Marumo Gallants ya Afrika Kusini imeshuka daraja kutoka Ligi kuu ya DStv kwenda ligi ya Motsepe Foundation Championship kufuatia kipigo cha 2-0 dhidi ya Swallows FC katika mchezo wa kufunga pazia la Ligi kuu Afrika Kusini.
Klabu ya Marumo Gallants ya Afrika Kusini imeshuka daraja kutoka Ligi kuu ya DStv kwenda ligi ya Motsepe Foundation Championship kufuatia kipigo cha 2-0 dhidi ya Swallows FC katika mchezo wa kufunga pazia la Ligi kuu Afrika Kusini. Marumo Gallants imemaliza msimu ikiwa mkiani nafasi ya 16 alama 29 baada ya mechi 30 na imeshuka daraja baada ya kuwa na msimu bora kwenye michuano ya Afrika ambapo ilifika nusu fainali kabla ya kuondoshwa na miamba ya Tanzania, Yanga SC.