Tue, 25 Apr 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Uongozi wa timu ya Marumo Gallants ya Afrika Kusini Umetangaza kuwa hakutakuwa na kiingilio katika mchezo wao wa marudiano dhidi ya Pyramids ya Misri,
Uongozi unafanya hivyo ili kuongeza nguvu ya mashabiki kuhakikisha kuwa wanasonga mbele kwenda Nusu fainali ya kombe la Shirikisho Afrika.
Matokeo ya kwanza Marumo wakiwa ugenini nchini Misri walitoa sare ya bao 1-1 huku wakiwa na Imani ya kufanya vizuri wakiwa nyumbani kwao Afrika Kusini.
Mshindi kati ya Marumo Gallants na Pyramids atakutana na Mshindi kati ya Yanga na Rivers United katika hatua ya Nusu fainali.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live