Thu, 4 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Patashika ya mashindano ya Kombe la Mapinduzi inaendela leo kwa michezo miwili.
Yanga iliyopo kundi C itakamilisha mechi za makundi itakapomenyana na KVZ kwenye uwanja wa New Amaan Complex.
Nazo Mlandege na Chipukizi za kundi A zitakiwasha katika mchezo utakaotangulia kwenye uwanja huo huo.
Katika michezo miwili ya michuano hiyo iliyofanyika Januari 3, Simba imeichapa Singida Fountain Gate mabao 2-0 wakati APR imeibuka mshindi dhidi ya JKU kwa mabao 3-1.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live