Klabu ya Yanga imesema imekusanya mapato ya shilingi bilioni 21.19 katika msimu wa mwaka 2023/24 ikijumuisha mapato ya mlangoni TZS bilioni 1.49, ada za wanachama TZS milioni 613, zawadi za ushindi TZS bilioni 3.46, udhamini na matangazo TZS bilioni 10.16 pamoja na mapato mengine TZS bilioni 5.45.
Aidha, imesema bajeti ya msimu ujao ni TZS bilioni 24.5.
MATUMIZI YA YANGA SC 2023/2024
7.39 bil Mishahara
3.5bilioni Usajili na uhamisho wa wachezaji
2.89bilioni Usafiri, Chakula na Malazi
1.85bilioni Maandalizi ya mechi
2.6bilioni Motisha kwa wachezaji na benchi la ufundi
702 Mil. Gharama za kambi
944 Mil. Compliance
1.46 Bil. Gharama za kiutawala
424 Mil. Gharama za masoko
503 Mil. Gharama za kifedha
Jumla Bil. 22, 288, 207, 535.