Mon, 20 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wakati Simba na Yanga zikifuzu na kuingia Robo Fainali Michuano ya CAF huku wakibakisha mchezo mmoja kwa kila timu hatua ya Makundi.
Mastaa wa vikosi hivyo wanaounda Timu ya Taifa wameshaanza safari kuelekea nchini Misri Kujiunga na Timu tayari kwa kuwakabili Uganda mchezo wa kufuzu AFCON.
Miongoni mwa mastaa hao ni mlinda mlango namba moja wa Stars Aishi Salum Manula ambae kupitia ukurasa wake wa Istagram ameandika;
"Nasemaaaje ni time ya national team kwenda AFCON baada ya vilabu vyetu kwenda robo finally"
Taifa Stars watashuka dimbani kukipiga na Uganda Machi 24 nchini Misri.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live