Juventus imeibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji AC Milan katika dimba la San Siro kwenye mchezo wa Ligi Kuu Italia Serie A na kukwea mpaka nafasi ya tatu ikifikisha alama 20 baada ya mechi 9.
Goli la pekee la ushindi katika mchezo huo limewekwa wavuni na Manuel Locatelli dakika ya 63'
MAAJABU: Mnamo Oktoba, 22 2016, Manuel Locatelli akiwa AC Milan alifunga bao mnamo dakika ya 65 na kuisaidia AC Milan kushinda 1-0 dhidi ya Juventus kwenye mchezo wa raundi ya 9 dimba la San Siro.
Jana Oktoba 22, 2023 Manuel Locatelli akiwa Juventus, amefunga bao mnamo dakika ya 63 na kuisaidia Juventus kushinda 1-0 dhidi ya AC Milan kwenye mchezo wa raundi ya 9 dimba la San Siro.