Tue, 1 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwenyekiti wa Klabu ya Simba SC, Murtaza Mangungu amewapiga dogo wapinzani wao wa jadi Yanga SC kwa kuwambia kuwa wameiga wazo lao la Simba Day.
Mangungu ameyasema hayo leo Agosti Mosi, 2023 alipokuwa Buza jijini Dar kulipokuwa na shamrashamra za kuelekea Simba Day.
"Tukio hili la Simba Day wengine wameiga ingawa hawataki kukiri hilo. Wameondoa neno Day wameweka Wiki," alisema Mangungu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live