Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Manchester United na dau la pauni milioni 40 kumnasa João Gomes

Manchester United Na Dau La Pauni Milioni 40 Kumnasa Gomes Manchester United na dau la pauni milioni 40 kumnasa João Gomes

Fri, 22 Mar 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Manchester United wanapanga dau la pauni milioni 40 msimu wa joto kumnunua kiungo wa Wolverhampton Wanderers João Gomes, kwa mujibu wa Mirror.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 amekuwa kwenye rada za United msimu huu, huku miamba hao wa Premier League wakituma maskauti kumtazama mchezaji huyo mara kadhaa.

Inaripotiwa kuwa huku Casemiro akitarajiwa kuondoka Old Trafford msimu huu wa joto, Mashetani Wekundu wanatamani sana kupata kiungo mkabaji, huku Gomes akitajwa kuchukua nafasi ya Mbrazil huyo.

Casemiro amekuwa na wakati mgumu katika kuwa na uthabiti msimu huu na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 huenda akaondoka United, ambao wanataka kuchukua nafasi ya mchezaji huyo wa zamani wa Real Madrid na mchezaji mchanga zaidi. Hata hivyo, dili halitakuwa moja kwa moja kwa Man United.

Ripoti hiyo inafichua kuwa wanaweza kukabiliwa na ushindani kutoka kwa Tottenham na Newcastle kwa ajili ya Mbrazili huyo, huku kuondoka kwake Wolves kukionekana kuwa kuna uwezekano baada ya klabu hiyo ya Midlands kuanza kubaini wachezaji watakaochukua nafasi hiyo kabla ya majira ya kiangazi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live