Thu, 25 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Manchester United ambayo kwa sasa haina Kocha baada ya kumtimua Ole Gunnar Solskajaer wiki iliyopita, imeanzisha mazungumzo na Mjerumani Ralf Rangnick kuja kuziba nafasi ya Ole Gunnar mpaka mwisho wa msimu.
Rangnick amewahi kuvifundisha vilabu vya Hoffenheim, RB Leipzig vinavyoshiriki Ligi kuu ya Ujerumani maarufu kama Bundasliga.
Rangnick kwa sasa anafanya kazi kama mkurugenzi wa maendeleo ya soka katika klabu ya Lokomotiv Moscow ya nchini Urusi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live