Wed, 8 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Manchester City inatazamia kumwajiri Lord Pannick KC ambaye ni mmoja wa Wanasheria wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson, kuisaidia klabu hiyo katika kesi ya kisheria dhidi ya Ligi kuu England.
Kwa kawaida Pannick hutoza pauni 5,000 kwa saa lakini anaweza kuitoza Manchester City pauni 80,000 kwa siku ikiwa kesi hiyo itafanyiwa hukumu.
Mshahara huo atakaolipwa Pannick KC ni sawa na mshahara wa Kevin de Bruyne.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: