Sun, 9 Jun 2024
Chanzo: Mwanaspoti
Nyota wa zamani wa soka Sunday Manara Computer’ anaendelea vyema baada ya upasuaji wa goti wa mguu wake wa kulia.
Manara ambaye alitamba kwenye soka la Tanzania miaka ya 1970 na mwanzoni mwa 1980 akichezea Yanga na timu ya Taifa, amethibitisha kuwa upasuaji huo umekwenda vizuri huku akiwapongeza Madaktari wa Hospitali hiyo.
Kadhalika, amewashukuru Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete na Mkurugenzi Mkuu wa Muhimbili Prof. Mohamed Janabi kwa kumuwezesha kufanikisha upasuaji huo.
Tunakuombea upone haraka Legend Sunday Manara Computer’
Chanzo: Mwanaspoti