Msemaji wa Yanga, Haji Manara ambaye anatumikia adhabu ya kufungiwa kutojihusisha na masuala ya soka kwa miaka miwili amefunguka kuhusu adhabu hiyo na masuala mengine yanayoendelea kwake.
Manara alifungiwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) mwaka jana baada ya kubainika kuwa alitoa lugha zisizo na staha kwa Rais wa TFF, Wallace Karia wakati wa fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam msimu 2021/22 kati ya Yanga dhidi ya Wagosi wa Kaya, Coastal Union.
“Naumia sana na kulaumu Serikali kukaa kimya sakata langu na TFF ilhali mi ni mwanaCCM na 'Pro Government' sijawai kuwa hata mpinzani bora hata angekuwa Mpinzani angefanyiwa haya Ila mi CCM,” amesema Manara.