Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Manara: Semeni ukweli Baleke harudi

Manara X Baleke Manara na Baleke

Mon, 10 Jul 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Akiwa ameaga Tanzania na kurejea nyumabni kwa DR Congo, Straika wa Simba Jean Baleke ameacha sintofahamu kubwa kwa mashabiki wa soka nchini.

Uongozi wa Simba SC umesema kuwa mchezaji huyo amekwenda kubadili Paspoti yake kwa kuwa imejaa huku wapo wanaosema ameachana na Klabu ya Simba ambayo alikuwepo kwa mkopo.

Sasa aliyekuwa Afisa Habari wa Klabu ya Yanga, kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;

"Nguo ya kuazima haistiri Tako

Acheni kudanganya kafata Passport eti imeisha muda wake, au imejaa.

Mpeni chake kama mlivyokubaliana vinginevyo mnajua connection yetu na Kinshasa.

Yaani Mtu karudi juzi Dar asijue passport yake imeisha au imejaa?

We give you only 24 hours otherwise mtavuna mabua, Ndegelec ,,

Nb: Sina kifua mm nawajuza mapemaaaaaa Congo tuna branch kule ya MGS

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: