Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Manara: Nilifungiwa kwa sababu ya Simba

Haji Manara Mazembe Manara: Nilifungiwa kwa sababu ya Simba

Mon, 27 Nov 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Aliyekuwa Msemaji wa Klabu ya Yanga, Haji S Manara amefunguka kuhusu sakata lake la kufungiwa na Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) baada ya kudaiwa kumtolea maneno machafu Rais wa Shirikisho hilo, Wallace Karia.

Manara alifungiwa kujihusisha na soka kwa muda wa miaka miwili na faini ya Tsh milioni 10 tangu Julai 2022.

“Kwanza TFF wananidhulumu wao wanajua ,nchi inajua na kila mtu anajua lile tukio nilifanya mbele ya watu sikumtukana nimemwambia siondoki hili unanifanyia mara nyingi ,nilimjibu hivyo Karia ule ni mradi tu na mimi nakwambia nimefungiwa kwa sababu ya Simba “

“Hata ripoti yao inaeleza hakukuwa na matusi ,majibizano ndio umfungie mtu miaka miwili na milioni 20 ,mimi ni muungwana sijakukosea lakini nikaenda kumuomba radhi nyumbani kwake,” amesema Manara.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: