Klabu ya Manchester United inakwenda kumenyana na klabu ya Nottingham Forest kwenye mchezo wa nusu fainali wa kombe la Carabao Cup.
Klabu ya Manchester United imefanikiwa kuting hatua ya nusu fainali baada ya kuifunga klabu ya Charlton 3-0 Huku klabu ya Nottingham Forest wao wakifanikiwa kuitoa klabu ya Wolves kwa mikwaju ya penati kwenye hatua ya robo fainali.
Manchester United imekua kwenye ukame wa makombe kwa miaka takribani miaka sita sasa huku wakitazamiwa kufanya lolote ndani ya msimu huu chini ya kocha Erik Ten Hag. Man United ilibeba taji lake la mwisho mwaka 2017 likiw taji la Europe League chini ya kocha Jose Mourinho.