Sun, 21 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Manchester United imethibitisha kuwa, Ole Gunnar Solskjaer ameachia ngazi kama Kocha ndani ya klabu hiyo.
Hatua hiyo imekuja baada ya ya siku ya jumamosi kupoteza kwa kipigo cha magoli 4-1 dhidi ya Watford.
Mchezaji wa zamani wa Klabu hiyo, Michael Carrick ndie atakaeshika nafasi kwa sasa katika michezo ijayo wakati Klabu ikitafuta kocha wa muda kuelekea mwisho wa msimu.
Manchester United watacheza mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya siku ya Jumanne dhidi ya Villareal ya Hispania.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live