Manchester United wako tayari kuongeza juhudi zao za kumsajili nyota wa Tottenham Harry Kane.
Gazeti la Telegraph linadai kuwa Mashetani Wekundu wanapanga kuwasilisha ombi la kumnunua nahodha huyo wa Uingereza, ambaye anaingia mwaka wa mwisho wa mkataba wake na hakuna uwezekano wa kusaini mpya.
Mwenyekiti wa Spurs Daniel Levy sasa atakabiliwa na uamuzi wa kuuza mali ya klabu hiyo au atamruhusu kuondoka bure mkataba wake utakapokamilika mwishoni mwa msimu ujao.
Manchester wanajua hawawezi kumudu sakata la uhamisho na wana hatari ya kukosa walengwa wengine kama vile Victor Osimhen wa Napoli kwa hivyo wanataka kufanya biashara yao mapema.
Imependekezwa Spurs itakuwa tayari kusikiliza ofa za pauni milioni 80 kutoka ng’ambo kwa Kane mwenye miaka 29, lakini itadai angalau pauni milioni 100 kutoka kwa vilabu vingine vya ligi kuu ya Uingereza.
Ripoti katika gazeti la The Sun linaonyesha kuwa Manchester United wako tayari kumpa mshambuliaji huyo mkataba mnono wa pauni 300,000 kwa wiki ili kumnasa Old Trafford. The Red Devils wana uhakika wa kumpata Kane ikiwa Spurs itamaliza nje ya nafasi nne za juu na hilo sasa linaonekana kuimarika baada ya kuchapwa 6-1 Jumapili na Newcastle.
Spurs watawakaribisha United walio katika nafasi ya nne siku ya Alhamisi wakiwa nyuma kwa pointi sita katika mbio za kufuzu kwa fainali ya Ligi ya Mabingwa.