Klabu ya Manchester United imemkatalia nyota wake Alejandro Garnacho kujiunga na kikosi cha timu ya Taifa ya Argentina kwa ajili ya michezo ya Olympic.
Klabu ya Manchester United imemkatalia nyota wake Alejandro Garnacho kujiunga na kikosi cha timu ya Taifa ya Argentina kwa ajili ya michezo ya Olympic. Michezo hiyo inatarajiwa kufanyika July 26, 2024 huko Paris nchini Ufaransa. Hii inakuwa sio timu ya kwanza kumkatalia nyota wake kwani inasemekana hata Klabu ya Real Madrid ipo mbioni kumzuia nyota wake Kylian Mbappe ambae anatarajiwa kutangazwa muda wowote kutoka sasa kujiunga na Ufaransa.