Mon, 10 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Manchester United imepata pigo katika jitihada za kusaka mrithi wa Eric Ten Hag baada ya kocha Thomas Tuchel kuamua kupumzika kufundisha soka kwa muda na hatakuwa kocha wa timu yoyote kwa sasa.
Fabrizio Romano anaripoti kuwa Tuchel ameamua kusitisha mazungumzo na klabu hiyo baada ya pande hizo mbili kukutana mara kadhaa hivi karibuni.
Tuchel alikuwa mmoja wa makocha wanaopigiwa upatu kukinoa kikosi hicho ikiwa Mashetani hao Wekundu wataamua kumuonesha Ten Hag mlango wa kutokea.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live