Droo ya hatua ya 16 bora ya Kombe la FA England imetoka huku vilabu 16 vikibaini wapinzani wao katika raundi ya 5 ya kombe hilo.
Manchester United itawakaribisha Wagonga Nyundo, West Ham katika dimba la Old Trafford huku Manchester City ikisafiri ugenini kwa vibonde Bristol City.
Tottenham Hotspur watakuwa wageni wa mmoja kati ya Wrexham au Sheffield United ambao bado hawajamalizana baada ya mchezo wa raundi ya 4 kumalizika kwa sare.
DROO KAMILI
Southampton vs Luton Town/Grimsby Town
Leicester City vs Blackburn Rovers/Birmingham City
Stoke City vs Brighton & Hove Albion
Wrexham/Sheffield United vs Tottenham Hotspur
Fulham/Sunderland vs Leeds United
Bristol City vs Manchester City
Manchester United vs West Ham United
Ipswich Town/Burnley vs Sheffield Wednesday/Fleetwood Town