Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Man United wanatumai kumpa mkataba mpya Ten Hag

'Huu Ni Mwisho Wa Ten Hag   Hakuna Kurudi Nyuma' Man United wanatumai kumpa mkataba mpya Ten Hag

Tue, 25 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Manchester United wanatarajia kukubaliana kandarasi mpya na Erik ten Hag kabla ya kuanza kwa ziara yao ya kujiandaa na msimu mpya nchini Marekani, chanzo kiliiambia ESPN.

United wamefanya mazungumzo na Ten Hag kuhusu kuongeza mkataba wake baada ya kuamua kumbakisha Mholanzi huyo kama meneja msimu ujao.

Vyanzo vimesema kwamba mazungumzo ni “magumu”yanayoendelea kati ya klabu na kocha huyo wa miaka 54 “yameendelea vizuri”.

United wanatarajia kufikia makubaliano kabla ya ziara yao ya kujiandaa na msimu mpya nchini Marekani ambayo itaanza na mchezo dhidi ya Arsenal mjini Los Angeles Julai 27.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live