Tue, 27 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Manchester United iko tayari kusikiliza ofa kwa mshambuliaji wao Antony katika majira ya joto.
Winga huyo alisajiliwa kwa kitita cha €95m akitokea Ajax mwaka 2022 mpaka sasa amekua na kiwango cha kusuasua tofauti na matarajio ya Manchester United.
Pia mmiliki mpya Sir Jim Ratcliffe anapanga kupunguza bili ya mishahara Old Trafford huku kwenye orodha hiyo majina kama Casemiro na Raphael Varane wakitarajiwa kuondolewa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live