Sat, 29 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Manchester United imetupilia mbali ofa ya West Ham United ya pauni milioni 20 kwa ajili ya kumsajili mlinzi wa kati, Harry Maguire.
Maguire (30) raia wa England ambaye alipokonywa kitambaa cha unahodha wa Man United bado anataka kusalia klabuni hapo kupambania kurejea kwenye kikosi cha kwanza.
Vilabu vya Chelsea, Newcastle United na Tottenham Hotspur vimeripotiwa kuhitaji saini ya beki huyo ghali zaidi katika historia ya soka.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live