Fri, 16 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Manchester United imepata ushindi wa 2-0 ugenini dhidi ya wenyeji, FK Sheriff Tiraspol katika mchezo wa Kundi E michuano ya UEFA Europa League jana Uwanja wa Stadionul Zimbru mjini Chisinau.
Mabao ya Manchester United yamefungwa na Jadon Sancho dakika ya 17 na Cristiano Ronaldo kwa penalti dakika ya 39, huo ukiwa ushindi huo kwanza na sasa wanazidiwa pointi tatu na vinara, Real Sociedad baada ya wote kucheza mechi mbili.
Kwa upande wao, Sheriff wana pointi tatu pia, huku Omonia Nicosia ambayo haina pointi inashika mkia
Chanzo: www.tanzaniaweb.live