Mon, 12 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Manchester United imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji, Aston Villa katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Jumapili Uwanja wa Villa Park, Birmingham.
Mabao ya Manchester United yamefungwa na Rasmus Hojlund dakika ya 17 na Scott McTominay dakika ya 86, wakati bao pekee la Aston Villa limefungwa na Douglas Luiz dakika ya 67.
Kwa ushindi huo, kikosi cha kocha Mholanzi, Erik ten Hag kinafikisha pointi 41, ingawa kinabaki nafasi ya sita kikizidiwa pointi tano na Aston Villa baada ya wote kucheza mechi 24.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live