Sun, 8 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wenyeji, Manchester United wametoka nyuma na kushinda 2-1 dhidi ya Brentford FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Jumamosi Uwanja wa Old Trafford Jijini Manchester.
Kiungo Mdenmark, Mathias Jensen alianza kuifungia Brentford FC dakika ya 26, kabla ya kiungo Mscotland, Scott McTominay kuifungia mabao mawili Manchester United dakika za nyongeza baada ya kutimia dakika 90 za kawaida (90'+3 na 90'+7).
Kwa ushindi huo, Manchester United inafikisha pointi 12 na kusogea nafasi ya tisa, wakati Brentford FC inabaki na pointi zake saba nafasi ya 14 baada ya wote kucheza mechi nane.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live