Sat, 19 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wenyeji, Tottenham Hotspur wameibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Manchester United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Tottenham Hotspur Jijini London.
Mabao ya Tottenham Hotspur yamefungwa na kiungo Msenegal, Pape Matar Sarr dakika ya 49 na beki Muargentina, Lisandro MartÃnez dakika ya 83 huo ukiwa ushindi wa kwanza kwao baada ya sare ya 2-2 na Brentford ugenini.
Kwa upande wao Manchester United leo wamepoteza mechi ya kwanza baada ya kuanza na ushindi wa 1-0 nyumbani dhidi ya Wolverhampton Wanderers.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live