Mon, 7 Mar 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha Mkuu wa Manchester United Ralf Rangnick amesema kuwa walikuwa bora kipindi cha kwanza lakini wakashindwa kuzitumia nafasi ambazo walizipata.
Rangnick amesema:"Nadhani tulikuwa bora kipindi cha kwanza lakini tumepoteza mchezo ni wajibu wetu kuweza kujipanga kwa ajili ya mechi zijazo.
United jana ilipoteza kwa kuchapwa magoli 4-1 Riyad Mahrez na Kevin De Bruyne wakiingia kambani mara mbili kila mmoja, huku goli la United likifungwa na Jadon Sancho.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live