Ligi Kuu England inaendelea leo kwa michezo sita ukiwemo kati ya Manchester United na Chelsea , unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa mpira wa miguu.
Manchester United ipo nafasi ya saba katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi 24 baada ya michezo 14 wakati Chelsea ni ya 10 ikikusanya pointi 19.
Katika michezo 78 ya mwisho timu hizo zilipokutana Manchester United imeshinda mara 23, zimetoka sare mara 32 wakati Cheslea imeshinda mara 23.
Michezo mingine ya EPL leo pamoja na Ligi Kuu Ufaransa ni kama ifuatavyo:
PREMIER LEAGUE
Brighton vs Brentford
Crystal Palace vs Bournemouth
Fulham vs Nottigham Forest
Sheffield United vs Liverpool
Aston Villa vs Manchester City
LIGUE 1
Marseille vs Lyon.
MATOKEO YA JANA
Wolves 1-0 Burnley
Luton 3-4 Arsenal
Goli la dakika za lala salama la Declan Rice liliwapatia Arsenal alama zote tatu na kuendelea kujichimbia kileleni kwa pointi tano zaidi kwenye msimamo wa Ligi Kuu England.