Thu, 19 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mamelodi Sundowns imesukumizwa nje ya michuano ya #CarlingKnockoutCup kufuatia kipigo cha penalti 5-4 dhidi ya TS Galaxy kwenye hatua ya 16 bora.
TS Galaxy wametinga hatua ya robo fainali baada ya kuiondosha Sundowns iliyokuwa pungufu ya mchezaji bora. Mchezo ulimalizika 2-2 mpaka muda wa ziada kabla ya matuta kuamua hatma ya Mamelodi Sundowns.
Sundowns wameondoshwa kwa matuta kwenye michuano ya pili mfululizo baada ya kipigo dhidi ya Orlando Pirates kwenye fainali ya MTN 8.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live