Mabingwa watetezi wa Kombe la Mapinduzi, Simba SC wamepangwa Kundi C pamoja na Mlandege na KVZ michuano ya Kombe la Mapinduzi inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi January 01 hadi 13, 2023.
Kwa upande wao, Yanga SC wao wamepangwa Kundi B pamoja na Singida Big Stars na wenyeji, KMKM ambao pia ni mabingwa wa Ligi Kuu ya Zanzibar kama ilivyo kwa Yanga kwa Tanzania Bara.
Kundi A linaundwa na Azam FC, wenyeji, Malindi SC na Jamhuri FC ya Pemba, huku Kundi D likiwa na Namungo FC, Aigle Noir ya Burundi na Chipukizi ya Pemba.
Group A 1:Azam FC 2:Jamhuri FC 3:Malindi SC
Group B 1:Yanga SC 2:KMKM 3:Singida Big Stars
Group C 1:Simba SC 2:KVZ 3:Mlandege
Group D 1:Namungo FC 2:Aigle Noir 3:Chipukizi