Mazungumzo kati ya Mshambuliaji wa kimataifa wa Zambia, Kennedy Musonda na klabu ya Yanga SC yanaendelea na yamefikia hatua nzuri ili kuachana na mshambuliaji huyo dirisha lijalo la uhamisho kuelekea msimu ujao.
Inatajwa Kennedy Musonda ataachwa ili apishe nafasi ya mshambuliaji mpya wa Yanga ambaye wamemalizana nae mpaka sasa, jina la mshambuliaji ambaye limeorodheshwa ili kupisha usajili mpya kwa nafasi ya Ushambuliaji ni Musonda na mazungumzo yapo almost 85%.
Kutokana na hilo klabu ya Yanga inaangalia kumtoa kwa mkopo Kennedy Musonda au kumuuza moja kwa moja kwasababu bado ana mkataba unamalizika msimu ujao.