Fri, 24 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Itikadi na Uenezi Comrade Paul Makonda leo ametimiza ahadi yake ya kuwapa ng’ombe watano Yanga SC baada ya kuibuka na ushindi mnono dhidi ya Simba SC, Nov 05.
Ng’ombe hao walipakizwa katika gari maalum na walitokea Lumumba Jijini Dar es Salaam zilizoko Ofisi za chama hicho na kupelekwa Jangwani yaliko Makao Makuu ya Yanga SC.
Ng’ombe hao wamekabidhiwa Yanga SC na wasaidizi wa Makonda walioko ofisini hapo Lumumba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live